Mwilu Kukagua Ujenzi Wa Mahakama Mpya Mombasa
Kaimu jaji mkuu Philemona Mwilu anatarajiwa kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na idara ya mahakama humu nchini.
Mwilu anatarajiwa kukagua mradi wa ujenzi wa mahakama mpya mjini Mombasa kabla na kukutana na wakuu wa idara ya mahakama kaunti ya Mombasa wakiwemo majaji na mahakimu katika harakati za kuboresha idara hio pamoja na utendakazi wao.